Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu, vyanzo vya kuaminika vimeripoti kuwa kituo cha kijeshi cha Marekani kilichopo katika jimbo la Hasakah, magharibi mwa Syria, kimelengwa na shambulio la makombora.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, makombora ya kutengenezwa nchini Iran yalilenga kambi hiyo ya kijeshi ya Marekani iliyoko eneo la Al-Shadadi.

Hata hivyo, mifumo ya ulinzi ya anga ya Marekani ilifanikiwa kuyazuia makombora hayo kabla hayajaleta madhara yoyote.

Baada ya shambulio hilo, hatua kali za kiusalama ziliimarishwa katika lango kuu la kuingilia kambini humo, huku wanajeshi wa Marekani wakionekana kuchukua tahadhari zaidi ili kuhakikisha usalama wa eneo hilo unaendelea kudhibitiwa.

Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu majeruhi au uharibifu wowote uliosababishwa na shambulio hilo.

Tutaendelea kufuatilia taarifa zaidi kuhusu tukio hili.

MiddleEastCrisis


Alikataa kuolewa ili amkomboe mama yake... Lakini mama ndiye aliyemuuza!

GORYANAH –Hii ni story ya Moto Sana yenye hisia na Mafunzo, binti jasiri anayepambana na siri nzito, umaskini na hatari kubwa kwa ndoto zake! Pakua app yetu ufurahie Sehemu ya 1 Hadi ya 5,na mwendelezo wake kila JUMAMOSI SAA MOJA KAMILI JIONI BURE!

BONYEZA HAPA KU DOWNLOAD.

Ukiona ujumbe wa allow notification bonyeza allow ili uwe mwanafamilia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *