Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemkosoa Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, akimtaka aache tabia ya “kuruka ruka” na badala yake afanye kazi ya kuwatumikia wananchi wa jimbo lake.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Wilayani Meatu, Mkoani Simiyu, Rais Samia alisema Mbunge Mpina ameshindwa kuwatetea wananchi wa Kisesa ipasavyo bungeni na badala yake anataka ajitafutie umaarufu wa kisiasa. Alifafanua kuwa miradi ya maendeleo imetekelezwa Kisesa, lakini Mbunge huyo amechagua kupuuza hilo.
“Ndugu zangu maombi kama haya kuyaleta hapa kwenye mkutano kwa Rais, ni kujitafutia umaarufu na kuthibitisha kwamba Mbunge hakulifanyia haki jimbo lake. Angeasema bungeni kazi hii ingefanyika, kwa sifa alizozitoa na maelezo aliyoyatoa. SGR, Mwalimu Nyerere, Daraja la Busisi, MV Mwanza — huyu si Mbunge wa jimbo bali wa Taifa, kwahiyo nadhani tunapokwenda huko muache nimchukue kwenye nafasi zangu kumi.
Alikataa kuolewa ili amkomboe mama yake... Lakini mama ndiye aliyemuuza!
GORYANAH –Hii ni story ya Moto Sana yenye hisia na Mafunzo, binti jasiri anayepambana na siri nzito, umaskini na hatari kubwa kwa ndoto zake! Pakua app yetu ufurahie Sehemu ya 1 Hadi ya 5,na mwendelezo wake kila JUMAMOSI SAA MOJA KAMILI JIONI BURE!
Ukiona ujumbe wa allow notification bonyeza allow ili uwe mwanafamilia.