Bosi wa DP World Ajiuzulu Kufuatia Kuhusishwa na Kashfa ya Mafaili ya Jeffrey Epstein

Mkuu wa waendeshaji wa bandari za kimataifa DP World ameiacha kampuni hiyo baada ya shinikizo kubwa kuhusu uhusiano wake na mkosaji wa ngono aliyehukumiwa Jeffrey Epstein.

Kuondolewa kwa Sultan Ahmed bin Sulayem kama mwenyekiti na mtendaji mkuu kunakuja baada ya faili mpya zilizotolewa kuonyesha kuwa tajiri huyo wa Imarati anaonekana kubadilishana mamia ya barua pepe na Epstein kwa muongo mmoja.

Kutajwa kwenye faili sio ishara ya makosa yoyote, na BBC imewasiliana na Sulayem kwa maoni.

DP World alitangaza kujiuzulu kwake, “kuanza mara moja”, siku ya Ijumaa, akimtaja Essa Kazim kama mwenyekiti na Yuvraj Narayan kama mtendaji mkuu. Picha ya Sulayem ilionekana kuondolewa kwenye tovuti yake.

Nyaraka hizo zinaonyesha kile kinachoonekana kuwa uhusiano wa karibu na mpana kati ya mmoja wa wafanyabiashara mashuhuri zaidi wa Ghuba na Epstein.

Zinaonyesha kwamba Epstein alimtambulisha Sulayem kwa watu mbalimbali wa kimataifa kutoka siasa na biashara kwa barua pepe, na kwamba Sulayem alimpa Prince of Wales ziara ya DP World’s London Gateway port mwaka 2016.

BBC

Related Posts