
Dakika 25 za kwanza timu zote mbili hazikuwa na umiliki mzuri wa mchezo , hakuna usahihi wa pasi , wanatupa mipira kirahisi sana ( hakuna game management ) .
βπΌ Yanga na muundo wao kama kawaida wakiwa na mali 2-1 then FBs wao wanakuwa pembeni zaidi ya kiwanjani dhumuni ni kuongeza machaguo ya pasi zao na kuwafanya Namungo kuzuia eneo kubwa la uwanja na walifanikiwa .
βπΌ Uwepo wa Maxi na Duke kama namba 8 wawili au 10 wawili ilitoa msingi sahihi kwa Yanga kuunganisha pasi zao vizuri tatizo likawa ni nini ?
A) Hakuna mchezaji mwenye uwezo wa kutengeneza nafasi eneo la mwisho badala yake wakawa wanatumia mawinga wao kushambulia β Half Spaces β kuifungua Namungo .
B) Namungo bila mpira wanakuwa na wachezaji wengi eneo la nyuma , maana yake Yanga wanatakiwa kuwa na mchezaji mwenye uwezo wa kupasia mpira vizuri kwenda mbele ( walikosa mtu kama huyo ) .
βπΌ Nafikiri kocha wa Namungo β Juma Mgunda β alijua kabisa hawezi kupishana na Yanga , alichokifanya ni kuzuia na idadi kubwa ya wachezaji then wanashambulia kwa kushtukiza . ( waliongeza Utulivu , usahihi wa pasi zao na uthubutu wa kushambulia nafasi eneo la mbele ) Kuna nyakati quality ndio iliwaangusha na idadi ndogo ya wachezaji eneo la mbele .
NOTE :
1: DEPU anafunga goli lake la nne ndani ya NBCPL : amefunga kwenye kila mchezo .
2: Ile ya Maxi ni Clear Penalty β Namungo walistahili kupewa tuta .
3: Okello anatakiwa kuboresha game yake ( mipira inapoteza kirahisi sana ) .
4: Maxi Nzegeli , Duke Abuya na Camara wametengeneza muunganiko mzuri kwenye kiungo ( timu ikiwa na mpira na bila mpira ) .
5: Job na Bacca ameshinda mipambano yao vizuri sana ππ½
FT : Namungo 0-1 Yanga Sc
By Kelvin Rabson
