Shilole Apata Ajali Mbaya ya Gari Baada ya Kugonga Ngombe

Rafiki wa karibu wa staa wa Bongo Fleva, Shilole, Baba Levo, amefunguka kuhusu tukio la kusikitisha lililotokea jana usiku.

Shilole alipata ajali ya gari aina ya Alphard wakati akirudi Dodoma kutoka Kigoma, baada ya kugonga ng’ombe katika eneo la Maragalasi.

Baba Levo amesisitiza kuwa wanamuangalia Shilole kwa karibu na kwa sasa anaendelea kupokea matibabu. Mashabiki wake wanashauriwa kuendelea kumuombea.

Tunafuatilia kwa karibu hali yake ya afya na tutaendelea kutoa taarifa mpya pindi zitakazopatikana.

Related Posts