Kocha Benchikha Akalia Kuti kavu JS Kabylie

Aliyekuwa kocha wa Simba Sc, Abdelhak Benchikha anakalia ‘kuti kavu’ ndani ya Klabu yake JS Kabylie ya Algeria baada ya klabu hiyo ya Ligi kuu Algeria kuambulia pointi 6 tu kwenye mechi 5 za Ligue 1 huku ikikamata nafasi ya 10 kwenye msimamo.

Taarifa kutoka Nchini humo zinaeleza kwamba kocha huyo wa zamani wa USM Algers amepewa mechi 3 tu za kujiuliza kabla ya kutupiwa virago ikiwa klabu hiyo itaendelea kuwa na mwenendo usioridhisha.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *