
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema tayari Wizara yake imeanza kuangalia uwezekano wa kumpatia uraia Kiungo Mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama kufuatia kiwango kikubwa ambacho ameendelea kukionyesha ndani na nje ya Nchi.
Akizungumza katika usiku wa Tuzo za BMT 2025, zinazofanyika leo Mei 09, 2026 Superdom Masaki Jijini Dar es salaam, Makonda amesema kiwango cha hivi karibuni alichoonyesha nyota huyo, hasa bao lake la kuvutia katika mchezo uliopita, kimeifanya Wizara kuanza kuona namna ambavyo anaweza kuwa sehemu ya kuongeza nguvu ndani ya kikosi cha Taifa Stars kuelekea mashindano mbalimbali ya kimataifa.
“Kwa lile goli la juzi, Wizara imeanza mchakato wa kuona taratibu za kumpatia uraia Chama ili kuongeza uwezo wa Timu yetu ya Taifa,” amesema Makonda
