RASMI: Sensor Mbatha CEO Mpya TRA United

Aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa zamani wa klabu za Simba SC ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ na Yanga SC ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ, Senzo Mbatha Mazingiza ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฆ, ametangazwa kuwa Mtendaji Mkuu mpya wa klabu ya TRA United FC ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ.

Senzo, ambaye ana uzoefu mkubwa katika uongozi wa soka barani Afrika, amewahi kufanya kazi na vilabu vikubwa kama Yanga na Simba SC, ambako alisaidia kuimarisha miundombinu ya kiutawala na mafanikio ya ndani na kimataifa.

Ujio wake ndani ya TRA United unatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika usimamizi wa klabu hiyo, hususa katika upande wa utawala na uendeshaji, huku lengo likiwa ni kuijenga timu hiyo kuwa miongoni mwa vilabu vinavyoshindana vikali kwenye ligi kuu ya NBC.

โšฝ๐Ÿ”ฅ Karibu tena Tanzania Senzo Mbatha!

Related Posts