Spika TuliaSpika Tulia

Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson amewataka wabunge wanaoongea na simu bungeni kutoka nje ya ukumbi wa bunge kwani wanatumia sauti kubwa ambayo inaondoa utulivu katika vikao vya bunge.

Dkt. Tulia alifafanua kuwa anafahamu kuwa kuna wabunge wanakabiliwa na usumbufu wa wajumbe majimboni na amewasisitiza kuwa kama wanahitaji kuzungumza vizuri, ni bora waende nje ya ukumbi wa bunge.

“Wale mnaoongea na simu mnaanza kidogo kidogo lakini baadae sauti zinapanda sijui wajumbe wanawasumbua huko lakini waheshimiwa wabunge ambao ni lazima mzungumze na simu naomba muende nje” Dkt. Tulia Ackson – Spika wa Bunge la Tanzania

Agizo hili lina lengo la kuboresha mazingira ya utulivu na ufuatuliaji wa kikao cha bunge kinachoendelea ili wabunge waweze kuzingatia mjadala unaoendelea wa Hali ya Uchumi wa Taifa na Bajeti kuu ya serikali.


Alikataa kuolewa ili amkomboe mama yake... Lakini mama ndiye aliyemuuza!

GORYANAH –Hii ni story ya Moto Sana yenye hisia na Mafunzo, binti jasiri anayepambana na siri nzito, umaskini na hatari kubwa kwa ndoto zake! Pakua app yetu ufurahie Sehemu ya 1 Hadi ya 5,na mwendelezo wake kila JUMAMOSI SAA MOJA KAMILI JIONI BURE!

BONYEZA HAPA KU DOWNLOAD.

Ukiona ujumbe wa allow notification bonyeza allow ili uwe mwanafamilia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *