
Allan Okello ameendelea kung’ara katika Ligi Kuu, akijipambanua kama mmoja wa wachezaji hatari zaidi kwenye ubunifu wa pasi za mabao (assists).
Nyota huyo wa kimataifa amefika kileleni mwa orodha ya vinara wa kutoa pasi za mabao katika NBC Premier League, hatua inayodhihirisha mchango wake mkubwa kwenye timu yake na ushindani wa ligi kwa ujumla.
Kwa ubora wa maono yake uwanjani na uwezo wa kuamua mechi kwa pasi za mwisho, Okello ameendelea kuwa “star boy” anayevutia macho ya mashabiki na wadau wa soka nchini.
🔥 Je, ataweza kudumu kileleni hadi mwisho wa msimu?
