Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa ameeleza kuwa Wizara hiyo itaendelea kuwalinda Watanzania kwa kusimamia maudhui mbalimbali mtandaoni ikiwamo mitandao ya kijamii ili kuhakikisha sheria na taratibu za nchi zinafuatwa.
Silaa amesema hayo katika kipindi maalumu Cafetalk @cafetalk_tanzania kilichofanyika siku ya Jumapili Juni 22, 2025 wakati akijibu maswali ya jopo la wanahabari nguli kuhusu zuio la baadhi ya mitandao ya kijamii kama X kuzuiwa nchini Tanzania.
Ameeleza kuwa baadhi ya maudhui ya baadhi ya mitandao hiyo imekuwa ikikiuka sheria, kanuni, na utaratibu ambao taifa la Tanzania limejiwekea.
“Hauwezi ukaacha mila na desturi za nchi yetu, hauwezi ukaacha maadili ya taifa letu, huwezi sheria za nchi kuvunjwa, hata baa ipo kwa mujibu wa sheria”, ameeleza Silaa.
Alikataa kuolewa ili amkomboe mama yake... Lakini mama ndiye aliyemuuza!
GORYANAH –Hii ni story ya Moto Sana yenye hisia na Mafunzo, binti jasiri anayepambana na siri nzito, umaskini na hatari kubwa kwa ndoto zake! Pakua app yetu ufurahie Sehemu ya 1 Hadi ya 5,na mwendelezo wake kila JUMAMOSI SAA MOJA KAMILI JIONI BURE!
Ukiona ujumbe wa allow notification bonyeza allow ili uwe mwanafamilia.