Mshambuliaji wa zamani wa Yanga anayekipiga kwa sasa Tabora United, Yacouba Songne amesema amepeleka malalamiko Fifa, baada ya kutolipwa mshahara wa miezi minne na kutomaliziwa ada ya usajili. Yacouba ambaye alisaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia Tabora msimu huu, alipata majeraha katikati ya msimu jambo lililomfanya kukosa mechi nyingi.

Akizungumza na arena, nyota huyo alisema mkataba upo ukingoni Tabora United, lakini bado hajapewa malipo yake na pia hakumaliziwa kiasi cha ada ya usajili. “Nimeipeleka Tabora United Fifa kwa kushindwa kunilipa stahiki zangu, lakini pia sehemu kubwa ya matibabu yangu nje nalipa mwenyewe badala ya timu. Ukiachana na msharaha ambao sijaupata kwa takribani miezi minne, lakini pia hata ada yangu ya usajili sijamaliziwa mpaka sasa.” alisema Yacouba


Alikataa kuolewa ili amkomboe mama yake... Lakini mama ndiye aliyemuuza!

GORYANAH –Hii ni story ya Moto Sana yenye hisia na Mafunzo, binti jasiri anayepambana na siri nzito, umaskini na hatari kubwa kwa ndoto zake! Pakua app yetu ufurahie Sehemu ya 1 Hadi ya 5,na mwendelezo wake kila JUMAMOSI SAA MOJA KAMILI JIONI BURE!

BONYEZA HAPA KU DOWNLOAD.

Ukiona ujumbe wa allow notification bonyeza allow ili uwe mwanafamilia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *