KIKOSI cha SimbaKIKOSI cha Simba

Mokocha Yanga Waipa Ujanja Simba Fainali Kombe la Shirikisho Afrika

INAWEZEKANA. Ndivyo walivyosema kwa nyakati tofauti makocha wa zamani wa Yanga, Luc Eymael na Hans van der Pluijm wakiamini Simba inaweza kupindua matokeo ya mabao 2-0 dhidi ya RS Berkane katika mechi ya pili ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika itakayopigwa nchini wikiendi hii.

Vijana wa Fadlu Davids wanahitaji ushindi wa mabao 3-0 ili kuandika historia ya kutwaa taji hilo kwa mara ya kwanza baada ya kupoteza 2-0 mechi ya kwanza yaliyowekwa wavuni ndani ya dakika 14 za kwanza za pambano lililopigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Manispaa ya Berkane, Morocco.

Wakizungumza na Mwanaspoti jana, makocha hao walisema walivyotazama mechi ya kwanza wanaamini Simba bado ina nafasi ya kubadili matokeo kama itaonyesha nidhamu ya kiuchezaji, utulivu na ubunifu eneo la ushambuliaji.

Eymael ambaye kwa sasa anaifundisha Saint Eloi Lupopo ya DR Congo, alisema ubora muda mwingine si kigezo cha kuamua matokeo. “Berkane walikuwa bora zaidi katika dakika za awali, lakini baada ya dakika 20 Simba ilirejea mchezoni. Kama wangeanza na utulivu ule tangu mwanzo stori ingekuwa tofauti. Hili bado linawezekana,” alisema Eymael.

Kocha huyo alikumbushia Simba kwenye robo fainali dhidi ya Al Masry ambapo iliibuka na ushindi wa mikwaju ya penalti baada ya kukomboa mabao 2-0 ambayo iliruhusu katika mechi ya kwanza ya Cairo, Misri.

“Hiyo mechi iwe kumbukumbu kuwa Simba wakicheza kwa nidhamu na kasi wanaweza kupindua matokeo. Kwa namna nilivyowaona wana kikosi chenye wachezaji wa aina tofauti hivyo kila kitu kipo mikononi mwao japo haitakuwa rahisi. Wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii,” alisema Eymael.

Naye Hans Pluijm, kocha aliyeinoa Yanga kwa vipindi tofauti kisha kupita Azam na Singida Big Stars ambaye kwa sasa anaishi Ghana, alisema: “Simba wana faida ya kucheza nyumbani mbele ya mashabiki wao. Kama watamudu kupata bao la mapema moja tu basi sura ya mchezo itabadilika kabisa na presha yote itahamia kwa Berkane.”

Pluijm alisisitiza kuwa mechi hiyo siyo kwa wachezaji tu, bali pia benchi la ufundi kuwa na mbinu tofauti na zile ilizotumia pambano la kwanza kwa mechi nyingine:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *